Psalms 104:1-3

Kumsifu Muumba

1 aEe nafsi yangu, umhimidi Bwana.

Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana,
umejivika utukufu na enzi.
2 bAmejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,
amezitandaza mbingu kama hema
3 cna kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji.
Huyafanya mawingu kuwa gari lake,
na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Copyright information for SwhNEN